TENZI ZA ROHONI 007 NI TABIBU WA KARIBU

Discussion in 'Tenzi za Rohoni' started by Eliyyahu, Jul 3, 2018.

  1. Eliyyahu

    Eliyyahu Administrator Pastor

    Messages:
    304
    Likes Received:
    118
    Trophy Points:
    43
    1. Ni tabibu wa karibu;
    Tabibu wa ajabu;
    Na rehema za daima;
    Ni dawa yake njema.

    Imbeni, malaika,
    Sifa za Yesu Bwana;
    Pweke limetukuka
    Jina lake Yesu.


    2. Hatufai kuwa hai,
    Wala hatutumai,
    Ila kweli yeye ndiye
    Atupumzishaye.

    3. Dhambi pia na hatia
    Ametuchukulia;
    Twendeni na amani
    Hata kwake Mbinguni.

    4. Huliona tamu jina
    La Yesu Kristo Bwana,
    Yuna sifa mwenye kufa
    Asishindwe na kufa.

    5. Kila mume asimame,
    Sifa zake zivume;
    Wanawake na washike
    Kusifu jina lake.

    6. Na vijana wote tena,
    Wapendao sana
    Waje kwake wawe wake
    Kwa utumishi wake.
     

Share This Page